Kuendesha biashara ndogo kunahitaji maono juu ya shughuli za kila siku. Kutokana na muda pia kuwa kikwazo, inakuwa ni vigumu kufikiria mbele. Wakati huo huo, Ili uweze kufanikiwa unahitaji kujua mipango bora ya mbeleni pamoja na athari zinazoweza kujitokeza. Karne ya 21 imekuja na mabadiliko makubwa ambayo yanaweza kuathiri biashara ndogo katika siku zijazo. Je, umeiweka wapi biashara yako katika kipindi cha karne ya 21?

Takwimu zinaonyesha zaidi ya 81% ya watu sasa hufanya utafiti wa biashara Fulani au huduma kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Hii inafanya kuwa zaidi ya watu Milioni 25.92 ambao utafuta biadhaa au huduma mtandaoni. Hii ni idadi kubwa mno kama unamiliki biashara.

Mteja wa karne ya 21 hanunui bidhaa au huduma bila kuwa na uhakika nayo. Mara nyingi huwa hawana Imani kama biashara haipo kwenye mfumo wa mtandao au kwenye website. Kwa maana nyingine, the 21st century consumer is a skeptic.

Deep Media Digital Agency kupitia tafiti zao za kibiashara, imebaini kuwa kuna ulazima wa biashara kumiliki tovuti (Website) ili kuweza kuendana na tabia za mteja wa karne ya 21.

Kwanini website?

Kwanza, Website itaifanya biashara yako iaminike na kila mteja wako (Add instant credibility). Hii ni kutokana na kuwa taarifa za bidhaa na huduma zako zote zinapatikana kwa urahisi ambazo hmara zote hujibu maswali yote ya mteja kabla ya kufanya maamuzi.

Pili, kumiliki Website, kunaifanya biashara yako kuwa katika soko la ushindani (Marketing competition). Katika karne hii ya 21 ambapo watu wengi utafuta bidhaa mtandaoni kabla ya kufanya maamuzi ya kununua, unahitaji kuna na uwanja utakaokuwa unatoa kitu cha ziada tofauti na wengine. Hakuna kingine zaidi ya Website.

Lakini tatu, kumiliki website kwenye biashara yako kunajenga na kudhibiti jina la biashara yako (Build and control your brand). Kama utafanikiwa kuwa na tovuti basi utaweza kiujenga Imani kwa wateja wako, utaweza kujibu maswali ya wateja wako, utaweza kuwapa wateja wako wanachohitaji kwa wakati. Kujenga jina la biashara kunahitaji kutengeneza Imani kubwa kwa wateja wako.

Je, wewe umeshawahi kufikiria kuwa na website ya biashara yako? Biashara nyingi sasa zimeahamia huku. Kama kweli unahitaji kuingia kwenye soko la ushindani ni wazi hauwezi kuepuka. Deep Media Tanzania wanakutengenezea sio tu website bali website ambayo inatoa majibu ya biashara yako. Kwa mawasiliano zaidi bonyeza HAPA, au piga simu kwa namba hii hapa chini.

+255 758 259 234